KOMEDIAN ambaye pia alikuwa msanii
wa muziki wa Bongofleva, Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’ amefariki
dunia leo majira ya saa mbili usiku katika ajali ya gari. Sharo
amefikwa na mauti wakati akiwa safarini akitokea Dar es Salaam kuelekea
nyumbani kwao, Kijiji cha Lusanga, Muheza mkoani Tanga. Msanii huyo
alikuwa anaendesha gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili
T478 BVR na amepata ajali eneo la Songa- Maguzoni wilaya ya Muheza
mkoani Tanga. Marehemu alikuwa peke yake kwenye gari. Kamanda wa Polisi
Mkoa wa Tanga, Costantine Massawe amethibitisha kutokea ajali hiyo na
katika taarifa yake kwa vyombo vya habari saa chache baada ya ajali,
alisema kuwa mchoro wa ajali unaonesha kuwa gari la marehemu liliacha
njia kabla ya kupinduka mara kadhaa. Naye Mkuu wa Wilaya ya
Muheza, Subira Mgalu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kubainisha
kwamba gari alilopata nalo ajali limeharibika sana.
“Mimi sijafika eneo la tukio
lakini nimezungumza na OCD wetu hapa Muheza, Andrew Satta yeye alifika
eneo la tukio na kunipa taarifa kamili. Ukweli ni kwamba msiba huu ni
majonzi na pigo kubwa kwa Wilaya ya Muheza kwa sababu huyu kijana ni
mzawa wa hapa.
“Muheza
tulikuwa tunajivunia kipaji cha Sharo Milionea lakini hatuna jinsi,
kila kitu kinapangwa na Mwenyezi Mungu,” alisema Mgalu.
Tanzania has lost another irreplaceable talent, Gone too soon. R.I.P Sharo Milionea
Hivi ndivyo
linavyo onekana gari aina ya Toyota Harrier alilokuwa anaendesha
marehem Ramadhan Hassan aka Sharo Milionea mara baada ya kupata nalo
ajali na kusababisha kifo chake.
Hivi ndivyo gari hilo inassemekana linavyo onekana kwa mbele
(naomba mtuwie radhi imebidii tuondoe ile picha ya text maana inaelekea kuna mtu kaamua kujifurahishia na ujitunguia sms ionekane alikuwa anachat na marehemu lakini alikosea mda maana mda ulioweka tayari ndugu yetu alikuwa amesha angulia mbele za haki)
(naomba mtuwie radhi imebidii tuondoe ile picha ya text maana inaelekea kuna mtu kaamua kujifurahishia na ujitunguia sms ionekane alikuwa anachat na marehemu lakini alikosea mda maana mda ulioweka tayari ndugu yetu alikuwa amesha angulia mbele za haki)
HIKI NDO ALICHOKISEMA KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA KUHUSU KIFO CHA SHARO MILLIONEA
Taarifa Kuhusu kifo cha msanii/mwigizaji Sharo Milionea, namkariri
Kamanda wa Polisi Tanga akisema “leo majira ya saa mbili usiku kwenye
barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika kwa jina la Hussein
Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari namba T478 BVR Toyota
Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza alipofika eneo la
Maguzonizonga wilayani Muheza hilo gari lake liliacha njia na kupinduka
mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa
kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”
Kamanda amesema hakuna kona kali sana wala ubovu wa barabara kwenye
sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea, katikati ya Segera na Muheza
ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa sababu haitembei.Kwenye gari
alikua mwenyewe
YANAYOJIRI KWENYE MSIBA WA SHARO MILLIONEA:
Hali ya mzee King Majuto presha imepanda na hali kuzidi kuwa mbaya kutokana na kupata taarifa za msiba wa Sharo Milionea.
Mjomba
wa marehemu Sharo Millionea, Bwana Omary Fundikira asema marehemu
anatarajiwa kuzikwa siku ya kesho, Jumatano. Hii ni kutokana na msanii
mwenzake John Maganga kuzikwa leo.
Mkuu
wa polisi mkoa wa Tanga RPC Costantine Massawe asema Hussein Ramadhani
(Sharo Milionea) alikuwa mwenyewe katika gari na ilipotokea ajali gari
lilimrusha nje na kufariki hapohapo.
Pia
rafiki wa marehemu bwana Mohamed Ismail ambaye ndiye aliyemuazimisha
gari alilopata nalo ajali, asema ilitakiwa waongozane kwenda Tanga
pamoja ila alishindwa maana alipata majukumu mengine.
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !