Habari Zetu :

Home » , » MABADILIKO KIWANGO CHA UFAULU, SIFURI KWAHERI.

MABADILIKO KIWANGO CHA UFAULU, SIFURI KWAHERI.

Written By Unknown on Thursday, October 31, 2013 | 10:35 PM



Prof Sifuni Mchome

Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania imetangaza kufuta daraja sifuri katika matokeo ya elimu ya sekondari nchini na kuongeza daraja la tano ambapo pia matokeo ya kidato cha nne kwa watahiniwa wanaorudia mitihani yatahusisha matokeo yao ya awali wakati wakiwa shuleni ili kuwarahisishia kupata alama nzuri.

Katibu mkuu wa Wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi Profesa Sifuni Mchome amesema pamoja na marekebisho hayo pia wameongeza daraja B ya juu (B+) kwa alama za ufaulu ambapo daraja A kiwango cha ufaulu ni kati ya alama 75 na 100, daraja B la juu (B+) ni kati ya alama 60 na 74, daraja B la kati (B) ni 50 na 59, daraja C kati ya 40 na 49, daraja D kati ya 30 na 39, daraja E kati ya 20 na 29 na daraja F ni kati ya alama 0 na 19.

Profesa Mchome amesema marekebisho hayo yanalenga kuinua kiwango na kuboresha kiwango cha elimu Tanzania ambapo kwa kila mhitimu wa kidato cha nne matokeo yake ya mwisho yatachangia alama 60 yatajumlishwa na alama 40 ambazo zitatokana na majibu ya mitihani ya kidato cha pili, cha tatu na mtihani wa Mock.

“Alama A itakuwa ni ufaulu uliojipambanua, B+ itakuwa ni ufaulu bora sana, B ufaulu mzuri sana, C ufaulu mzuri, D ufaulu hafifu, E ufaulu hafifu sana na F ufaulu usioridhisha kabisa,” alisema Profesa Mchome.



Aliongeza pia kwa kusema kuwa, utaratibu wa sasa wa kupanga matokeo hayo kwa madaraja, utabadilika muda wowote kuanzia sasa na kwamba utakaokuwa ukitumika ni ule wa wastani wa alama katika ufaulu (Grade Point Average ‘GPA’).

Mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka huu utafanyika November 4, 2013 ambapo zaidi ya Watahiniwa laki nne wanatarajiwa kufanya mtihani hii ambapo kati yao, Watahiniwa laki 3 na elfu 67,399 ni kutoka shuleni huku Wavulana ni 198,257 sawa na asilimia 53.69 na Wasichana ni 169,142 sawa na asilimia 46.04 ambapo vituo vya kufanyia mitihani ni 4,365.



 
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

PROFESSIONAL BLOG DESIGNERS

PROFESSIONAL BLOG DESIGNERS

IDADI YA WATU

BLOG ARCHIVE

DROP YOUR COMMENTS HERE

 
Designed by : Bongo Blogs Designers | Bloggerized by | Tryphone Chasama Jr
Contacts: 0719 625003 / 0765 860437Welcome
Copyright © 2011. SNOUT HOT NEWZ - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template