MATOKEO KIDATO CHA NNE 2012 KUPANGWA UPYA
Serikali
imetangaza uamuzi wa kupanga upya matokeo ya kidato cha nne ya 2012.
Uamuzi huo umetangazwa mapema leo bungeni na Waziri William Lukuvi, kwa
niaba ya Waziri Mkuu. Uamuzi umetokana na kamati ya waziri mkuu
iliyokuwa inachunguza kuhusu matokeo hayo kubaini kuwa matokeo hayo
yalipangwa kwa utaratibu tofauti na uliokuwa unatumika zamani.
Tetesi za awali zilieleza kwamba matokeo hayo yalipangwa kwa kuzingatia
madaraja haya hapa chini, japo Baraza la Mitihani lilikanusha baadaye
kwa kusema kuwa taarifa hizo hazikuwa za kweli:
A = 80%-100%-
B = 65%-79%-
C = 50%-64%-
D = 35%-49%-
F = 0%-34%-
Tume ya Waziri Mkuu imebaini kutumika kwa madaraja tofauti na
uataratibu wa awali. Hivyo basi, matokeo yaliyotangazwa hayatatumika
tena mpaka yaje yaliyopangwa upya. HakiElimu itatoa taarifa rasmi
baadaye kuhusu uamuzi huu wa serikali.
Kila la kheri.
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !