Habari Zetu :

Home » , » UHURU KENYATTA ATANGAZWA RASMI KUWA RAIS WA NNE WA KENYA

UHURU KENYATTA ATANGAZWA RASMI KUWA RAIS WA NNE WA KENYA

Written By Unknown on Saturday, March 9, 2013 | 6:36 AM



Nairobi Kenya.
Uhuru Kenyatta wa muungano wa JUBILEE ametangazwa rasmi na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC Isaac Hassan kuwa mshindi wa urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika jumatatu ya tarehe 4/3/2013. Matokeo hayo yametangazwa baada ya majadiliano ya muda mrefu yaliyofanyika kati ya tume ya uchaguzi na mipaka na viongozi wa vyama vilivyokuwa vikiwania nafasi hiyo. Matokeo hayo yamemwacha haamini mpinzani wake mkuu Raila Odinga wa muungano wa CORD. 
Jumla ya kula zilizopigwa ni 12,338,667 kati ya wapiga kura 14,337,399 waliojiandikisha na waliokuwa na haki ya kupiga kura. Kenyatta amepata jumla ya kura 6,173,433 ambazo ni sawa na asilimia 50.03 dhidi ya mpinzani wake Odinga aliyepata kura 5,340,399 sawa na asilimia 43 ya kula zote. Matokeo hayo ndiyo yaliyomfanya Uhuru kutangazwa rasmi kuwa rais mteule wa awamu ya nne katika Jamhuri ya Watu wa Kenya,

Uhuru Kenyatta, on November 19
           Rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta

MATOKEO KWA UJUMLA NI KAMA IFUATAVYO;
1. Uhuru Kenyatta, JUBILEE  6,173,433
2. Raila Odinga, CORD      5,340,399
3. Musalia Mudavadi,  AMANI  483,981
4. Peter Kenneth, EAGLE  72,786
5. Abduba Dida, ARK  52,848
6. Martha Karua, NARK-K  43,881
7. James Kiyiapi, RBK   40,998
8. Paul Muite, SAFINA  12,580


Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

PROFESSIONAL BLOG DESIGNERS

PROFESSIONAL BLOG DESIGNERS

IDADI YA WATU

BLOG ARCHIVE

DROP YOUR COMMENTS HERE

 
Designed by : Bongo Blogs Designers | Bloggerized by | Tryphone Chasama Jr
Contacts: 0719 625003 / 0765 860437Welcome
Copyright © 2011. SNOUT HOT NEWZ - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template