Habari Zetu :

Home » , » MAUAJI KANO, NIGERIA

MAUAJI KANO, NIGERIA

Written By Unknown on Friday, February 8, 2013 | 10:36 PM



Ripoti kutoka nchini Nigeria zinasema kuwa watu 12 wakiwemo wafanyakazi waliokuwa wanatoa chanjo ya Polio kwa watoto, wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.
Maafisa wa afya wameiambia BBC kuwa wafanyakazi wanane waliokuwa wanatoa chanjo waliuawa mjini Kano,na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Walioshuhudia mauaji hayo wanasema kuwa, watu wengine 8 waliuawa katika kituo cha afya maeneo ya Hotoro, karibu na mji wa Kano.
Miongoni mwa waliouawa ni wanawake waliokuwa wanawasubiri watoto wao, waliokuwa wanachanjwa.
Baadhi ya viongozi wa kiisilamu, Kaskazini mwa Nigeria wamekuwa wakipinga chanjo ya Polio, wakisema inasababisha watu kukosa uwezo wa kuzaa.
Source; BBC
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

PROFESSIONAL BLOG DESIGNERS

PROFESSIONAL BLOG DESIGNERS

IDADI YA WATU

BLOG ARCHIVE

DROP YOUR COMMENTS HERE

 
Designed by : Bongo Blogs Designers | Bloggerized by | Tryphone Chasama Jr
Contacts: 0719 625003 / 0765 860437Welcome
Copyright © 2011. SNOUT HOT NEWZ - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template